Tafuta Hapa / Search here

Loading...

Saturday, 18 May 2013

NDOA YA DIAMOND PLATNUMZ NA PENNY YANUKIA.

Maharusi watarajiwa Dimaond Platnumz & VJ Penny
Esma Abdul ambae ni dada yake mwimbaji staa wa Tanzania, Diamond Platnums, amesema wamejiandaa vizuri kwa ajili ya harusi ya Diamond ambae anatarajiwa kumuoa mtangazaji wa TV aitwae Penny.

Esma ambae anaishi nyumba moja na kaka yake amesema, "Tumemkubali sana wifi yetu na tunampenda kwa sababu mtu yeyote mimi nitakaetambulishwa siwezi nikamkataa, manake nikimuingilia kwenye mapenzi yake na yeye ataniingilia kwenye mapenzi yangu."

Huu ni mwezi wa tano toka Esma amjue wifi yake ambae ni Penny, anasema nyumbani amekubalika na mipango ya harusi inaandaliwa japo hajui ni lini itafanyika, manake hiyo ni siri kwa sasa.
Dada yake Diamond aka wifi yake Penny
Zaidi ya wiki tano zilizopita, Diamond aliongea na kusema ndoa yake imekaribia kufungwa na huyo mkewe mtarajiwa ambae ni mjamzito lakini pia akathibitisha kumnunulia gari la kutembelea aliloliagiza nchini Japan - Hyundai IX 35.

Mpaka sasa Mwimbaji Diamond Platnums ambae aliongoza kwa kuwa msanii wa Tanzania alieandikwa sana kwenye internet 2012, ameshaingia kwenye headlines za kuwa mapenzini na mastaa wa kike Tanzania kipindi cha nyuma kama Jokate, Wema Sepetu na wengine. 

Source: Millard Ayo

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

SPOTTED: SOLANGE KNOWLES AT THE 66TH ANNUAL CANNES FILM FESTIVAL.

Solange Knowles was one of the red carpet stars at the 66th Annual Cannes Film Festival after showing up to The Great Gatsby premiere rocking this Stéphane Rolland dress. The usually color-friendly star opted to tone down her eccentric style by rocking a neutral color, still managing to stun onlookers in the process.


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

VIDEO: 2 CHAINZ & WIZ KHALIFA - "WE OWN IT

2 Chainz and Wiz Khalifa don’t appear in the music video for ‘We Own It’, taken from the upcoming soundtrack of Fast & Furious 6. But it’s still a nice montage of scenes from the movie which opens on Memorial day. The soundtrack, which hits stores on May 21st is available for pre-order. Watch the action heavy visual below.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

Friday, 17 May 2013

Video: Fat Joe – ‘Ballin’ (Feat. Wiz Khalifa & Teyana Taylor)

Fat Joe is prepping the release of his new album The Darkside Vol. 3 and today, he premieres the video for his latest single ‘Ballin’ featuring Teyana Taylor and Wiz Khalifa

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

TID aka MNYAMA NAE AITOLEA NJE SHOW YA LADY JAY DEE.

Show ya miaka 13 katika muziki ya Lady Jaydee inazidi kupata pigo baada ya TID kuwa msanii mwingine latest kujitoa kwenye show hiyo.
Hivi ndivyo alivyoandika TID kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

PERONI JAZZ SUNDAY AT VELISA'S

Jumapili hii Mei 19 kuanzia saa Kumi na Moja jioni hadi Saa Mbili usiku karibu uburudike na muziki laini wa Jazz ukiletwa kwako na Wakwetu Jazz Vibes pamoja na mpiga gitaa nguli, Jessie. Njoo ujumuike na marafiki pamoja na jamaa wengine Velisa’s Beach. Usisahau kuwaambia na wenzako.



Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

FLAVIANA MATATA FOR TRUWORTHS.




U go girllllllllll

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

MUSIC: SIKILIZA NYIMBO 4 MPYA KUTOKA KWA "LINEX, MB DOG, OPG MAJINGX NA BWANA MISOSI FT DULLAYO"



Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

CHRISTINA AGUILERA - BACK TO BEING HOT.

Christina Aguilera is back to work and looking red hot while at it. The pop icon posted a photo of herself shooting the music video for her new single with Alejandro Fernandez called “Hoy Tengo Ganas de Ti.” In the photo, Xtina looks flawless while showing off her recently slimmed down body. She dons a black bra and skirt and strikes a diva pose with a gorgeous view in the background.
Shooting music videos isn’t the only thing Xtina is making a return to. She’s just been confirmed to return to her big, spinning red chair for season five of The Voice. Christina and fellow coach Cee-Lo Green stepped away for season four, making way for new coaches Shakira and Usher to fill in.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

TANGAZO LA AJIRA KATIKA NCHI ZA AFRIKA KWA WATANZANIA WALIOPO UINGEREZA NA MAJIRANI.

CAREERS IN AFRICA INAWATANGAZIA WALE WOTE WENYE SHAUKU YA KUTAFUTA KAZI BARA LA AFRIKA KUHUDHURIA KONGAMANO KUBWA LA KAZI LITAKALOFANYIKA JIJI LA LONDON KUANZIA TAREHE 17 MPAKA 19 MEI , 2013.
CCM UK -TUNAOMBA KUWATANGAZIA WATANZANIA WOTE, BILA YA KUJALI ITIKADI ZAO ZA KISIASA, KUJIANDIKISHA NA KUHUDHURIA KWA WINGI KONGAMANO HILI KWA KUJITAFUTIA AJIRA, AMA HATA KUJIFUNZA MENGI MAZURI YATAKAYOJIRI.
KWA MAELEZO ZAIDI NA JINSI YA KUJIANDIKISHA TAFADHALI TEMBELEA TOVUTI YA: www.careersinafrica.com

NAWATAKIA KILA LA KHERI

MARIAM MUNGULA
KATIBU CCM - UK

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

MWANAFUNZI WA DARASA LA KWANZA AFARIKI KWA KUANGUKIWA NA MBAO DAR ES SALAAM (HABARI).

Gorofa linalojengwa katika eneo la Ilala Bungoni mtaa wa mafuriko jijini Dar es salaam bila kufuatasheria ya kuweka vizuizi kwa ajili ya usalama wa watu,imesababisha kifo cha mwanafunzi wa darasa la kwanza mwenye umri wa miaka 6 baada ya kupigwa na mbao yenye misumari iliyorushwa kutoka juu ya ghorofa hilo na kufariki papo hapo.


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

JENNIFER LOPEZ OPENS UP ON HER RELATIONSHIP WITH CASPER SMART SAYING IT IS "SWEET" & "HEALTHY"..

Jennifer Lopez, who has been married three times, has said that she will "probably" tie the knot again. 

The Latino singer was previously married to singer Marc Anthony, dancer Cris Judd and actor Ojani Noa. She currently dates choreographer Casper Smart, who is 18 years her junior. 

"I like marriage," said the former American Idol judge. "I like the idea of it; I always have. As a girl you never really give up on that fairytale completely." 

Jennifer, 43, also told Entertainment Tonight that her relationship with Casper, 25, was "sweet" and "healthy". 

Jennifer has admitted that the breakdown of her seven-year marriage to Marc was hard, particularly as her five-year-old twins Emme and Max ask a lot of questions. 

"They ask hard things. They'll say, 'Didn't Daddy used to live here? When is he coming back to sleep here. And I say, 'Yes he did, but he has his own home now.' I just try to make it okay for them because that's all I care about. I don't want to damage them in any way." 

In an interview with People earlier this year, she admitted that she worried that current boyfriend Casper might stray in ten years time. "I ask him, 'Why don't you go find a young girlfriend and get out of here?'" she admits. "'What do you want with me?' And you think, 'How long is this gonna be?' 

The truth is we don't know what's going to happen. We're loving this moment right now. We make each other happy." 

"He's fantastic; he's like my best friend," she has said. "I can tell him everything, when I'm feeling down, when I'm feeling good. 

"He gives moral support, endless love and support." Jennifer recently showed off her enviable beach body in the music video for new single Live it Up.


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

WEMA SEPETU KUSHIRKI BIG BROTHER AFRICA? HAYA NI MAONI YA BAADHI YA WADAU.

Hivi ndivyo mjadala ulivo anza kupitia ukurasa wangu wa facebook:

"Kuna tetesi kwamba beautiful Onyinye wetu Wema Sepetu anatarajia kuingia katika jumba la Big Brother Africa mwaka huu. Binafsi kama hizi habari ni za ukweli nadhani itahit sana kwa yeye tu kuingia humo na itapata viewers wengi sana je wewe unamoni gani au ungependa kumuona nani katika hilo jumba la BBA? Onyo naomba msitukane hapa bali toeni maoni na mawazo yenu tu asanteni."  JwaD

Haya ya fuatayo ni baadhi ya maoni ya wadau


Faiza Ally 
Nimesikia pia - nahisi atafanya vizuri go girl

Bob Manase 
Nadhani ni right choice kikweli!

Femie Mgongolwa 
aminia!

Mboni Mhita 
Communication skills zake ni nzuri, as she has fluent english. Nadhani apart from that contestant anabidi awe na nidhamu, awe na uzalendo, na ajue muda wote kuwa ana wakilisha nchi yake, akumbuke primary goal ni kurudi na ushindi back home, na akumbuke ni mchezo na kila mtu amefuata ushindi,wengi wamekuwa wakijisahau na kuitumia kama platform ya kujitangaza, japo sio vibaya ila mtu asisahau sababu iliyo mpeleka. Na wasirubuniwe kirahisi...Whoever can pull this...I am all cool,

Ruth David Manento 
Amenyooka,,, na ung'eng'e upo hapo

Paul Kimiti 
Na iwe hivyo........itahit kulko zote

Debora Mkemwa 
akienda sawa, ila kwa tabia zake za kujiachia sana naogopa aibu kwa TZ.

Moses Ryakitimbo 
All the best for her! She is beautifull,also straight in english communication skills!afanikiwe. Nampenda

Lulu Komanya 
I second Mboni Mhita very true and very well said thanks

Andrew Sospeter 
Anafaa sana na cha msingi arekebishe makosa ya waliotangulia ili asimamishe Tanzania kidedea

Aney Sabry 
Lol

Daniel Owden EJ 
Wema Should go. If she wants to 
its not bad

Rachel A. Temu 
Good luck for her kama haitatokea wampe TID

Nkundwe Mwaipopo Wetengere 
Go girl, already you are star.


The Lilly Melody Show 
Akienda itakuwa Poa sana!!


Ebou Shatry 
Okay

Esir White Muhideen 
yy ndo atafit kutinga mjengoni...


Je wewe unamaoni gani juu ya jambo hili? 


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

TOP FASHION DESIGNERS SKETCH MATERNITY DRESSES FOR KATE MIDDLETON.

Kate Middleton already has one of the best-dressed bumps around. Her ability to recycle and perfectly mix high-street with couture established her place as a fashion favourite some time ago, and in the last few months she has been praised for her elegant maternity choices.

Now that the pregnant royal is really starting to show, some of the biggest names in the industry — no doubt itching to dress her growing tummy — have sketched suitable designs for the Duchess.
 

 Among those submitting their maternity ideas to style website WWD are Karl Lagerfeld, Nina Ricci, Donna Karen, Vera Wang and French fashion house Chloé.

German Chanel designer Karl, 77, has imagined a beautiful long-sleeved blue dress with a plunging neckline for Kate, while Donna opted for an elegant evening gown, perfect for a official evening outing. 
Chloe presented a summery ruffled peach frock, while Nina Ricci sketched a floral stretch silk printed crepe dress with black silk detailing.
 

 "Kate Middleton is elegant, sensual, timeless," the American designer wrote in her accompanying caption. "This is a dress she could wear forever, during and after her pregnancy."
 

 

So far, Kate seems to have stayed away from maternity wear, opting instead for loose-fitting clothing in her wardrobe — she recently recycled a black and white polka dot dress by high street favorites Topshop. Now though, with her beautiful bump growing ever bigger, perhaps she will consider stepping out in some of these latest fashion recommendations.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

LINAH, BARNABA KUTUPIWA VIRAGO THT.

Na *****************Andrew Chale
KUELEKEA shoo maalumu ya Miaka 13, ya mwanamuziki nguli wa bongo fleva nchini na kiongozi wa bendi yenye msisimko mkubwa ya ‘Machozi Band’, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ au Jide’  huenda kwa upande wa wasanii wa Nyumba ya Vipaji ya THT, Linah Sanga na Barnaba  mwaka huu ukawa mchungu kwao kufuatia kuwepo taarifa za kutimuliwa na uongozi wa juu.

Kwa mujibu wa vyanzo kutoka kwa mtu wa karibu wa Linah kilieleza kuwa mpaka sasa msanii huyo hana raha na wala hajui ataanza vipi katika harakati zake za kimuziki hasa kufuatia hivi karibuni kukacha shoo ya nguli Lady Jay Dee kwa shinikizo kutoka kwa wakubwa zake.

Hata hivyo, Linah inadaiwa uongozi wa juu umekaa kikao na hatua iliyofuatia kwenye kikao hicho ni kuwaondoa kabisa kwani huenda wakatia doa wasanii wenzao ndani ya kundi hilo.

“Juzi Lina,haikuwa kawaida yake maana hata alipopigiwa simu na ** kwa ajili ya hatua zingine alionekana kuw na hofu, na wala hakutaka kusikia ushahuri wangu ambao nilikuwa nikimhusia kuwa aachane na mawazo hayo kwani jambo analoliwaza huenda likaisha na hata maamuzi yatakayotoka yatakuwa ni kawaida” kilieleza chanzo kutoka kwa mtu wakaribu wa Lina, amabaye hata hivyo alisema kuwa huenda ukweli wa jambo ukawa hadharani.

Hata hivyo taarifa za ndani za uongozi wa THT zilibainisha kuwa mpango wao wa kuwashughulikia wasanii hao upo pale pale na taratibu zinafuata ilizisilete madhara kwa wasanii waliopo ndani ya THT  na watu wa karibu wanaoiunga THT.

“Wewe nani kakwambia kama tumewaadhibu Lina na Barnaba?, ndio kwanza tunakusikia wewe hizo taarifa,  sisi tunafanya mambo yetu wao waache wafanye yao tukiwa nao sie na tunaouwezo wa kuwatimua ilikulinda hadhi ya THT” Kilieleza chanzo hicho ambacho hata hivyo kutokana na usalama wa jina lake tumelihifadhi. Ambapo namba yake inaishia na**08.

Aidha, katika ‘ku-balance’ huondo kamili wa habari hizi wasanii hao wote walipotafutwa kwenye simu zao za mkononi lakini hawakuweza kuwa hewani kwa muda mrefu.. na hata alipopigiwa mtu wao huyo wa karibu naye alizima simu.

Katika kile kinachoeleza kupamba moto shoo hiyo, na kujaa kwa taarifa mbalimbali juu ya wasanii watakaopamba shoo ya miaka 13, Mei 31 ndani ya Nyumbani Lounge, Tayari tiketi zimeanza kuuzwa maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Saalam.

Shoo hiyo ya kijanja Nyumbani Lounge, patakuwa hapatoshi pale wadau wa burudani na wastaarabu wote watakapojumuika kwa pamoja ku-shoo love kwa Lady Jay Dee  na Machozi Band, huku listi ya mastaa mbalimbali wanatarajia kuudhuria sambamba na ‘surprise’ kutoka kwa mastaa hao ambao kwa sasa wengi wapo kimya wakihofia kutengwa na wazee wa ‘fitina bin Logiki’.

Awali kulikuwapo na taarifa za kuwapo kwa msanii Matonya, ambaye hata hivyo mtandao wa Lady Jay Dee ulitoa hadharani kuwa mwanamuziki huyo ameshachukua ‘advance’ ya shoo hiyo na wazee wa ‘kuingilia logik’ wameshamtisha Matonya ili ajitoe, lakini akiwa ameshatafuna pesa ya watu.
Mtandao huo wa kijamii  blog, ilinukuu kila kitu juu ya Makubaliano baina ya Capt.Gadna G Habashi na Matonya ambapo pia unaweza kuyasoma kupitia (Ladyjaydee.blogspot.com) Pia ulitoa kwa mara ya kwanza picha,maelezo muhimu na video ya wanamuziki hao wawili Linah na Barnaba wakiingia mkataba wa shoo hiyo na pia kuhamasisha watu kufika Mei 13..

**KWA TAARIFA ZAIDI  KWA KINA JUU YA BARNABA NA LINAH, usikose kuzisoma katika gazeti la Tanzania Daima ** Pindi watakapopatikana tutaweka hadharani kila kitu.

Mwisho

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

RIHANNA FOR RIVER ISLAND SUMMER COLLECTION.






Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

WARAKA WA 'ANTIVIRUS' KWENDA KWA RUGE NA KUSAGA. (1 of 88)

ANTiVIRUS DAWA YA Virus WA Hiphop in Tanzania
WARAKA NAMBA 1(ZIPO 88) KILA WIKI UTAPATA WARAKA MMOJA

Ni wazi na dhahiri kabisa kesi iliofunguliwa mahakamani dhidi ya Lady JayDee haina maana yoyote isipokuwa ni hofu ya mafisadi wa muziki nchini (Kusaga na Ruge) kwa kuwa waraka wa pili ulikuwa utoke tar 15 may na mwingine tar 17 may mwaka huu wa 2013.

Hapa la kujiuliza ni juu ya interview ya Rugen a kinachoendelea sasa,eti suala limefika mahakamani,kweli Kusaga na Ruge mmeweza kuthibitisha nyie ni mafisadi na mnamuaibisha Rais Kikwete ambaye nina uhakika anajua kuwa nyie ndio kikwazo kikubwa na hata Bungeni alishawahi kuzungumza kuwa alitoa studio na pango kumbe tatizo sio hilo,tujiulize wote kuna nini wanachoficha hadi kumtafutia kesi raia mwema asie na hatia?

Tena anaejitafutia rizki ambayo wao wanapigana nayo kwa kumkandamiza?

Huku wakitumia mabavu wakilindwa na baadhi ya viongozi wa serikali na waandishi ambao majina yao mtayapata kupitia nyaraka zinazokuja (zipo 88) na huu ndio wa kwanza.

Nimesikitika sana na njia pekee ya kuufahamisha umma juu ya ufisadi huu wa Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga ni kuyaanika yote ambayo jamii na Viongozi wa Serikali kama mlikuwa hamjui sasa ndio wakati muafaka wa kuwajua watu hawa ambao kila kukicha ni kuimarisha ufisadi wao na kujipendekeza kwa Viongozi sambamba na watoto wao (mtajua mpaka majina yao)

Naanza kupatwa na wasiwasi nikijiuliza, endapo Lady JD angekuwa amegombana na msanii mwenzake mkubwa kama Prof Jay, Ray C au Juma Nature wanasiasa wangeingilia kati? Ni wazi wasingesogea kwa kuwa hakuna maslahi zaidi ya kuingilia mgogoro huu ambao hawataki jamii ijue maovu yao.

Napatwa mashaka jinsi wanasiasa wanavyolivalia njunga jambo binafsi
Kama hili na kulifanya ni la kiserikali basi tafuteni chanzo cha tatizo mjue ni sehemu gani sahihi ya kuanza kutatua kilichopo na sio kukimbilia kuunda vikao ambavyo naamini vimeshaitishwa vingi sana lakini hakuna kilichosaidia.

Wanasiasa badala ya kutafuta sababu zinazofanya wasanii wanalalamika mnakimbilia kutatua mgogoro wa Ruge na JD ili kusuluhisha mambo yasiendelee kuongelewa jamii ijue uovu wa mafisadi hawa.
Haitasaidia kwa sababu wanaojua maovu ya hawa mafisadi Rugen na Kusaga ni wasanii wengi wakubwa na watu wengine binafsi (kumbukeni waraka zipo 88)

Vijana mnaowategemea katika kampeni zenu na mnawaita Taifa la kesho, lakini mnakubali waendelee kukandamizwa na kunyanyasika huku wakizidi kuwaneemesha kina Ruge na Kusaga.

Tatizo mnalijua kaeni na wasanii wote wawaelezee matatizo yao, msikae na wasanii ambao wanaamrishwa na kina Ruge. Sikilizeni kilio cha wasanii wengine pia na itafutwe njia ya kupata maoni ya kila mmoja na kuachana na watu wengine ambao wanaendesha mtandao wa ufisadi chini ya kivuli cha Ruge (Said Fella na Babu Tale) ambao mtapata kujua kila kitu kuhusu ufisadi wao na kinachoendelea (kumbuka waraka zipo 88).

Ruge Mutahaba amekuwa ni tatizo na janga la Kitaifa katika tasnia ya muziki kwa ujumla, amekuwa akiwagawa wasanii kwa kutumia redio Clouds kwa vitisho vya kutopigiwa nyimbo, au kwa danganyio la kufanyiwa promotion mpaka kwenye magazeti endapo tu utakuwa chini ya bawa lake.

Wasanii wamekuwa hawalipwi vizuri ili waendelee kumtegemea fisadi huyu.

Kwani wasanii wote wangekuwa na kipato cha kuweza kusimama imara leo hii kauli kama ya Lady JD ingezungumzwa karibu na kila mwanabongoflava.

Fred Kavishe (fisadi mwingine) ambae anasimamia Kili music awards yuko bega kwa bega na Ruge kudanganya wananchi nani ni bora katika tuzo hizo ili kulinda maslahi yao binafsi.

Na wao huchagua wale wasanii ambao hawana sauti za kudai haki yao ili wawatumie kadri wanavyotaka.Tuzo za Kili ni uozo mtupu.Imefikia wakati basata itoe vibali kwa wadau wengine wa muziki (nako kuna ufisadi)wasio na interest binafsi na wasanii wao, kuendesha hizi shughuli ili kukuza muziki.Kutokuwepo na tuzo zingine kunasababisha ionekane kuwa basata nao wamo kwenye mgao wa mabepari hao wanaoua sanaa ya Tanzania

JINSI RUGE NA KUSAGA WANAVYOTAWALA
Njia anayoitumia Ruge na Kusaga iko wazi, wao wana redio na hapo hapo wana wasanii wao.Hivyo promotion inabidi wafanyie wasanii wao ambao ni waoga ili waweze kuwatumia bila wasanii hao kufanya fyoko fyoko.

Wasanii wengine ambao sio chini ya Clouds kwa kuwa hawana jinsi nyingine ya kupata hela inabidi wainyenyekee Clouds wakiamini ndio njia pekee ya kuwapatia vipato.
Huku wakisubiri show moja ya fiesta ya kila mwaka.
Huko katika fiesta kuna wengine wanalipwa mpaka laki tatu na bado katika hiyo ili upangwe kwenye list ya kupanda jukwaani B12 nae lazima akate laki moja yake.
Hapo msanii anabakiwa na nini akirudi nyumbani?
Hivi laki tatu ni nini kwa maisha ya msanii?
Njia pekee ya kuwatawala ni kuwafanya waendelee kuwa maskini.
Leo hii mtangazaji wa redio ana sauti kuliko msanii.

Kwanini redio zingine hazilaumiwi? Ni kwa sababu hazijihusishi moja kwa moja na wasanii.Hilo ni kosa kubwa sana linalofanywa na Clouds au pengine ndio mtazamo wao walioamua kuufuata kwa sababu wanaamini Serikali ipo mikononi mwao.
Maisha na ajira za watoto wa watu ambao wengi hawajasoma wanategemea vipaji, mnayakatili bila huruma

Mwisho tumuombee Lady JD Mahakama imruhusu azungumze yote, kila mtu anataka kusikia sio siri Clouds, Ruge na Kusaga ni nyonya damu.
Mahakama itambue kuwa wanaojua maovu ya Rugen a Kusaga sio Lady JayDee pekee ni wengi mno na kama njia ya kukimbilia mahakamani ndio wameichagua basi ongezeni mahakama kwa kuwa tupo wengi tutakuja kuyaongea kuhusu mafisadi hawa wa Clouds (siku hizi wanaitwa wafu).

Hela ina nguvu hata palipo na haki, JD hajatukana matusi na amekuwa makini katika kutoa kauli zake sasa anashitakiwa kwa kosa gani? Anashitakiwa kwa kudai haki yake. Anaconda wewe songa na sisi tunakuja kizimbani na sasa ndio TANZANIA itawajua Rugen a Kusaga ni kina nani na walianzia wapi,walikuwa wapi,wako wapi na nani wanaoshirikiana nao, JIPANGENI!

SAIDIA KUSAMBAZA NENO.
MDAU



Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

TIKETI ZA MECHI YA SIMBA VS YANGA KUANZA KUUZWA KESHO, NANI KUCHEKA, NANI KUNUNA, NANI KULIA, ITAJULIKANA JUMAMOSI

Simba SC na Yanga FC kuchuwana Jumamosi
Nani kuficha mabango ya utani Jumamosi?
Tiketi kwa ajili ya pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Yanga litakalochezwa keshokutwa (Jumamosi) kwenye Uwanja wa Taifa zitaanza kuuzwa kesho (Ijumaa) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Vituo vitakavyouza tiketi hizo kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni ni Uwanja wa Taifa, mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, OilCom Ubungo, kituo cha mafuta Buguruni, BMM Barbershop Sinza Madukani, Dar Live Mbagala na Sokoni Kariakoo.
Tiketi hizo zitakuwa zikiuzwa katika magari maalumu yaliyoegeshwa katika vituo hivyo. Viingilio katika mechi hiyo ya kufunga msimu ni sh. 5,000 kwa viti vya kijani, sh. 7,000 viti vya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C, sh. 20,000 VIP B n ash. 30,000 kwa VIP A.
Mashabiki wa Yanga wakiwakebehi mashabiki wa simba
Mashabiki wa Simba wakijibu Shambulizi

Jee mashabiki wa Simba watakuwa na furaha kama hii jumamoso!!!???

Vipi Unahisi Camera Man Huyu wa Yanga Atakuwepo Uwanjani Jumamosi????

Nategemea Haitakuwa Hujuma Jumamosi hii!!!!!!!!!!



Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

TGT - SEX NEVER FELT BETTER {OFFICIAL VIDEO}

TyreseGinuwine and Tank give you the visual for their single, “Sex Never Felt Better,” the lead off from the group’s presently untitled debut album, which is slated to release some time later this year

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

NEW JOINT: HOT CANDY - NATASHA SHYROSE

Hot Candy is 3rd song on Natasha Shyrose album! Since she has using this song many times as promo track to get gigs, she decided to share with us! Are you ready for more? Full length album will be available on 1st June, 2013

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Mixed Posts