Tafuta Hapa / Search here

Loading...

Tuesday, 21 May 2013

SERENGETI FREIGHT FORWARDERS LTD

WAZEE WA KAZI

GOOD NEWS FOR TANZANIA
HUDUMA MPYA YA KIFURUSHI 
NEW DOOR TO DOOR SERVICE
TUNACHUKUA MZIGO MLANGONI KWAKO UK NA TUTAUFIKISHA MLANGONI KWAKO DAR
UKILIPA HAPA UK HAULIPI TENA DAR, SISI TUTAKULETEA MZIGO NYUMBANI KWAKO!
Baada ya kushughilikia kwa kina mapungufu yaliyojitokeza mwanzo, 
sasa tumerudi na huduma ya kifurushi tena ikiwa imeboreshwa zaidi.
BEI ZETU KAMA KAWAIDA HAZINA KIGUGUMIZI NA SI ZA KUUMIZA

AIR CARGO TO DAR NOW £3.50 INCLUSIVE CLEARANCE!
AIR CARGO TO ZANZIBAR NOW £3.00 INCLUSIVE CLEARANCE!
AIR CARGO TO NAIROBI/MOMBASA NOW £2.80 INCLUSIVE CLEARANCE!
KIFURUSHI KWA KONTENA DAR/ZANZIBAR NOW £2.20 INCLUSIVE CLEARANCE!

NDEGE ZINAONDOKA KILA WIKI MARA MBILI
TUNAFUATA MZIGO KUTOKA POPOTE UK
MINIMUM WEIGHT IS 40KILOS
KAMA UNATAKA KUAGIZA KITU AU KUFANYA BOOKINGS TUWASILIANE KWA NAMBA HAPA CHINI
CHRIS LUKOSI +44 07903828119  & 07404279633 
SIMON LOUIS (MOHSIN) +44 07950689243
HASSAN  +44 07448795075

HQ -  UNIT 92 THAMES INDUSTRIAL PARK, PRINCESS MARGARET ROAD, EAST TILBURY, RM18 8RHRH
 
*****WE NOW CHARGE £850 FOR 4X4 VEHICLES FROM TILBURY****

SERENGETI FREIGHT FORWARDERS LTD
UNIT 92 THAMES INDUSTRIAL PARK, PRINCESS MARGARET ROAD,
EAST TILBURY, ESSEX, RM18 8RH


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

A SNEAK PEEK OF IDRIS ELBA AS NELSON MANDELA IN NEW BIOPIC.

The long awaited and much anticipated autobiographical pic of anti-apartheid revolutionary Nelson Mandela, Mandela: Long Walk to Freedom, stars none other than Idris Elba.
The film is slated to hit theaters November 29, and sets out to convey the story of the South African leader and President from 1994-95 and his early life. It delves into his coming of age, education and 27 years of incarceration.
sneak peek arrives in the form of a poster via Yahoo, which sits up top. Stay tuned!


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

FLAVIANA MATATA ASHIRIKI MISA YA AJALI YA MV BUKOBA.

 Flaviana Matata akiwa Baba ake mzazi katika Misa ya  maombelezo  Ajali ya MV Bukoba ambapo Flaviana alimpoteza Mama yake mzazi, Igoma,Mwanza
Flaviana Matata akiwa ofisini kwa projest  Samson Kaija ambaye ni General Manager wa Marine Services Company ltd ambao hushurkiana nae katika maombolezo ya Ajali hii ambapo mwaka jana aliwapa msaada wa maboya ya kujiokoa
 Flaviana Matata akiwa na marafiki na baadhi ya waombolezaji waliopoteza ndugu zao katika ajali hiyo
Flaviana Matata akiwasha mshumaa ikiwa ni ishara ya kuomboleza katika Makaburi ya Igoma Mwanza walikozikwa baadhi wananchi walopoteza maisha yao miaka 17 iliyopita.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

HOT NEWS: PROFFESSOR JAY AJIUNGA RASMI NA CHAMA CHA CHADEMA.

TANZANIAN BONGO FLAVA LEGENDARY PROFESSOR JAY JOINED ‘CHADEMA POLITICAL PARTY TODAY’ AND HE HAS BEEN HANDED OVER THE MEMBERSHIP CARD FROM MEMBER OF PARLIAMENT JOSEPH MBILINYI (SUGU-BONGO FLAVA LEGEND) INFRONT OF HON JOHN MNYIKA AND HON WENJE

  Professor Jay, is a Tanzanian hip hop artist. He is one of the prominent representants of the "Bongo Flava" Tanzanian hip hop subgenre, which mixes elements from both Western hip hop and the Tanzanian tradition (including swahili lyrics as well as an activist attitude towards Tanzanian social issues such as HIV/AIDS, wealth, inequality, and political corruption).
 He started rapping in 1994 as a member of the group Hard Blasters, best known for their hit "Chemsha Bongo" (then he used stage name Nigga J) from their first album, "Funga Kazi". Only one year later, they won the title of best hip-hop group in Tanzania.
During his solo career which he started in 2001, he has released number of hits, including "Nikusaidiaje" and "Zali la Mentali (feat Juma Nature)". Other songs released by Professor Jay include "Piga Makofi" and "Yataka Moyo". Just like Mr. II, he is a pioneering Tanzanian MC, who have remained some of the most popular hip hop musicians in Tanzania, despite influx of many new bidders. Also similar to Mr. II his lyrics often have political messages. In one of his songs he imitates an elder politician and ridicules the fake promises they all mindlessly spew as they are trying to get elected. The song continues with a chorus saying the words "Ndio Mzee" which means "Yes Elder". This represents the brain washing of the public as politicians make these false promises over and over. It is interesting to note however, that after this song was produced, the president of Tanzania referenced the lyrics in one of his speeches, which acknowledged the presence of Bongo Flava and the success of Professor Jay's political lyrics. 
His first album, "Machozi, Jasho na Damu," gained instant recognition for which Professor Jay won several awards. He attained other awards such as the best hip-hop album in Tanzania with his second album, "Mapinduzi halisi".
Professor Jay's songs include Nikusaidiaje (featuring Ferooz), Nimeamini (featuring Lady Jaydee), Inatosha (featuring Sugu), Vuta raha (featuring Ferooz), Border kwa border (featuring Nazizi), Heka heka za star, Interlude, J.O.S.E.P.H., Nisamehe (featuring Banana), Wapi nimakosea, Una, Hakuna Noma, Jina Langu, Bongo Dar es Salaam, Piga Makofi, Msinitenge, Sio Mzee, Zali la Mentali, Nidivyo Sivyo, Mtazamo (featuring Afande Sele and Solo Thang), Hapo Sawa. Professor Jay is featured on Nonini's song "Kumekucha" 


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

OBAMA KUZURU SENEGAL, SOUTH AFRICA AND TANZANIA MWEZI WA JUNE.

Rais wa Marekani Barack Obama anatarajiwa kuzuru Senegal, Afrika Kusini na Tanzania mwezi Juni. Hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu ya White house
Rais Obama atakutana na watunga sheria na wafanyabiashara pamoja na viongozi wa asasi za kijamii.
Ziara ya Obama itaanza tarehe 26 Juni hadi 3 Julai na itakuwa ziara yake ya pili Kusini mwa jagwa la Sahara akiwa rais wa Marekani. Aizuru Ghana mwaka 2009
Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton na mwenzake George W Bush, wote walizuru Afrika wakati wa muhula wao wa pili wa utawala. Clinton alizuru nchi sita wakati Bush Alizuru nchi tano
''Rais atatilia mkazo uhusiano kati ya Marekani na baadhi ya nchi za kiafrika ambazo zinakuwa ikiwemo maswala kama ukuwaji wa uchumi, uekezaji na biashara pamoja na kukuza taasisi za kidemokrasia na kuendelea kukuza viongozi wa kizazi kijacho Afrika,'' ilinukuu taarifa kutoka ikulu ya White House.
Ziara ya Obama pia itatilia mkazo kukuza uhusiano kati ya Marekani na watu wa bara la Afrika ili kuendeleza ushirikiano wa kikanda, amani na ukuwaji.
Wadadisi wanasema kuwa ziara kama hizi hufanywa sana na marais wa Marekani hasa baada ya kuondokewa na kazi ngumu ya kampeini za uchaguzi na shinikizo za ndani ya nchi.
Wakati huohuo, tisho linaloongezeka kutoka kwa wapiganaji wa kiisilamu nchini Mali, limefanya kanda hiyo kumulikwa zaidi na Marekani. Bi Michel Obama ataambatana na mumewe katika ziara hiyo.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

UTAMBULISHO WA USIKU WA HIP HOP & FAINALI ZA VODACOM MIC KING KWA WANAHABARI.

Meneja Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kushoto) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho huo. Wengine pichani kutoka kushoto ni DJ John Dilinga (JD), Prodyuza Ally Baucha na Prodyuza Tudd Thomas.
Kutoka kushoto waliokaa ni msanii Stamina, DJ John Dilinga, Abdallah Mrisho, Ally Baucha na Tudd Thomas katika picha ya pamoja na washiriki wa The Vodacom Mic King waliosimama nyuma.
Wakali wa MIC wanaowania gari wakiwa katika pozi na gari hilo.
Wanahabari wakichukua baadhi ya matukio.
...Wakimsikiliza Abdallah Mrisho.
Hawa ndiyo wakali tisa wanaowania gari aina ya Toyota Funcargo (New Model)
-----------------------
Uongozi wa Dar Live Co. Ltd leo umetambulisha tamasha kubwa la kila mwaka la Usiku wa Hip Hop na fainali za kumtafuta Mkali wa Mic zijulikano kama 'The Vodacom Mic King' kwa wanahabari. Tamasha hili litafanyika Jumamosi hii, Mei 25, 2013 katika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar. Jumla ya vijana tisa wenye vipaji watapanda stejini kuchuana na mshindi ataondoka na gari aina ya Toyota Funcargo (New Model) yenye thamani ya shilingi milioni 15. Mbali na zawadi ya gari, mshindi wa kwanza, pili na watatu, watapata fursa ya kurekodi wimbo mmoja chini ya Prodyuza mahiri nchini, Tudd Thomas, aliyerekodi wimbo maarufu wa Leka Dutigite wa Kigoma All Stars na nyingine nyingi. Majaji katika shindano hili ni mwandishi mkongwe wa habari za muziki na wasanii, Abdallah Mrisho, DJ John Dilinga (JD) na Prodyuza Ally Baucha.
Tamasha hilo litapambwa na burudani kutoka kwa wakali wa Hip Hop nchini ambao ni Fid Q, Joh Makini, Stamina, Kala Jeremiah, Nay wa Mitego pamoja na shoo kali kutoka kundi la Wakali Dancers. Katika usiku huo, zitatolewa tuzo kwa wasanii wa Hip Hop na kwa wimbo bora wa Hip Hop uliofanya vizuri mwaka 2012/13. Kutakuwa na Tuzo kwa Msanii Mkongwe Bora wa Hip Hop na Msanii Chipukizi Bora wa Hip Hop pamoja na Wimbo Bora wa Hip Hop.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

TAMTHILIA: THE TEAM SEHEMU YA KWANZA NA YA PILI { EPISODE 1 & 2 }

Fuatilia hapa Tamthilia ya kiswahili the Team Kila siku Tutawawekea sehemu mbili mimi nimeipenda nategenmea na nyinyi watu wangu mtaipenda pia.


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

FAMILIA YA RAIS MWINYI MATATANI.


FAMILIA ya Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi imejikuta matatani kufuatia nyumba namba 13, kitalu 33F iliyopo Mtaa wa Mwinjuma, Kinondoni, jijini Dar anayoishi mjukuu wake, Abood Hassan Mwinyi kupigwa kufuli kwa amri ya mahakama.
Tukio hilo lilijiri saa 6:11 Jumamosi ya Mei 17, mwaka huu ambapo ilidaiwa Abood anaishi kwenye nyumba hiyo na mama mkwe wake bila uhalali.

Geti la nyumba anayoishi mjukuu wa Mzee mwinyi, Abood Hassan Mwinyi likiwa limepigwa kufuli
Edward Francis Bongwe ni mtoto wa aliyekuwa mmiliki na ndiye aliyeipiga kufuli nyumba hiyo akiwa ameongozana na Mjumbe wa Nyumba 10, Shina Namba 16, Zubeda Mrisho na Hariri Mohamed  anayedaiwa kuimiliki nyumba hiyo kwa sasa ambaye aliinunua kwa marehemu mzee Francis Mawenge.
Habari zinadai awali, mbali na Abood, mtoto wa Mzee Ruksa aitwaye Abbas naye alikuwa akiishi katika nyumba hiyo lakini baada ya kuuzwa kwa Hariri na kutakiwa kuhama, alitii agizo mapema kwa kwenda kuishi sehemu nyingine.
Novemba 7, mwaka 2011, Abood na Abbas walipewa notisi ya siku 90 kuhama katika nyumba hiyo chini ya Kampuni ya Uwakili ya LRK Chambers kupitia wakili wake, Richard Mmbando.

Abood Hassan Mwinyi akiwa nje baada ya nyumba kufungwa.
Barua hiyo yenye kumbukumbu namba LRK/GDM/NTC/0.045/011 iliwataka wawili hao ifikapo Februari 6, 2012 wawe wamehama lakini mpaka sasa Abood anaendelea kuishi humo huku akitambua kuwepo kwa barua hiyo.
Siku ya tukio, Edward ambaye pia ni msimamizi wa mirathi ya marehemu mzee Francis, akiwa ameongozana na Hariri na mjumbe, walimkuta mama mkwe wa Abood, Eshe Yassin ambaye alikuwa amembeba mtoto mchanga.
Alipojulishwa lengo la ujio huo, mwanamke huyo aliwazuia kutofunga kufuli mlangoni kwa vile hawakuwa na pa kwenda.
Alipoona hasikilizwi, Eshe alimpigia simu Abood na kumweleza kinachoendelea ambapo ilipofika saa 5:53, Abood alifika kwa kasi akiwa na gari dogo lenye namba za usajili T 572 BZU.
Hata hivyo, alishindwa kuingia ndani na gari hilo kwa sababu geti lilishapigwa kufuli. Akashuka na kuingia ndani ambapo alikuja juu baada ya kukuta zoezi la kupiga kufuli milango ya ndani likikaribia kuanza.

Baadhi ya wananchi waliofika eneo la Tukio. 
Hali ilikuwa tete na kukatokea vurugu kidogo baada ya Edward kumwamuru Abood kuhama muda huo ambapo kijana huyo alikataa kufanya hivyo, kitendo kilichoifanya familia ya marehemu mzee Francis kumfikisha mjukuu huyo wa rais mstaafu Kituo cha Polisi Oysterbay, Dar.
Alifunguliwa kesi ya jinai yenye Kumbukumbu OB/RB/8741/2013 KUJIPATIA HUDUMA KWA NJIA YA UDANGANYIFU.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi alionekana kituoni hapo muda mfupi baada ya Abood kufikishwa ikisemekana alitaka kujua kilichokuwa kikiendelea.
Kwa upande wake, Abood alipohojiwa na gazeti hili kutaka kujua kwa nini aliendelea kuishi katika nyumba hiyo wakati barua ya wakili ilimtaka awe ameondoka tangu Februari 6, 2012, alisema ana kila kitu, yaani vielelezo vya kumfanya aendelee kuishi. Hata hivyo, hakuvionesha!


Habari na Makongoro Oging wa GPL


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

WAYNE AND COLEEN ROONEY CELEBRATE BIRTH OF SECOND SON KLAY ANTHONY ROONEY

Manchester United star Wayne Rooney and his wife Coleen have had a second son, the couple announced today.
Mrs Rooney gave birth to Klay Anthony Rooney at 2.11am.Just hours later she tweeted the good news to her one million Twitter followers, saying:
Wayne Rooney also tweeted, to say the whole family was "delighted".
The couple announced in December they were expecting a son, two months after confirming Coleen's second pregnancy.
Coleen has previously admitted she would love to have a large family, saying: 'I'd like to have maybe three or four children. I'd be happy to be a full-time mum.'
Following in the footsteps of the Kardashians, the Rooneys could end up naming their future children with names beginning with K, after having Kai and Klay.



Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

FLAVIANA MATATA KUSHIRIKI KATIKA MISA YA KUMBUKUMBU YA MV BUKOBA.

Makaburi ya Igoma ambako ndugu zetu waliokuwa wakisafiri kwa meli ya MV Bukoba walizikwa.
Mwanamitindo, Flaviana Matata (wa pili kulia) akiomba dua katika kaburi la mama yake Mzazi maeneo ya Igoma mkoani Mwanza katika siku ya kukumbuka ajali ya MV Bukoba iliyoua watu takribani 1000 Mei 21, 1996.
Flaviana mbali na kukumbuka waliofariki katika ajali hiyo akiwamo mama yake mzazi pia alikabidhi msaada wa vifaa vya kuokolea maisha kwa Shirika la Kiserikali la Usafiri wa Maji Mwanza hapo mwaka jana.
Mwanamitindo wa kimataifa wa Tanzania, Flaviana Matata leo atashiriki katika misa maalum ya kuwakumbuka watanzania waliopoteza maisha katika ajali ya MV Bukoba mwaka 1996.
Misa hiyo itafanyika kwenye eneo la makabuli ya kumbukumbu ya MV Bukoba ambapo Flaviana alipoteza mama yake mzazi na kaka yake katika ajali hiyo.
Mwaka jana, mwanamitindo huyu kupitia shirika lake la Flaviana Matata Foundation alitoa msaada wa maboya yaani vyombo vya kuokoa maisha majini (life vests) 500 kwa mawakala wa meli ya serikali yaani Marine Services Ltd ikiwa ni nja moja ya kujaribu kusaidia usalama majini. 
Mkurugenzi wa kampuni ya Compass Communications, Maria Sarungi alisema kuwa mbali ya kushiriki katika misa hiyo, pia mwana mitindo huyo atafanya mazungumzo na wadau mbali mbali jinsi ya kuendeleza juhudi za kuimarisha usalama majini.
Flaviana alisema kuwa juhudi zake kubwa kwa hivi sasa ni kuhakikisha kuwa ajali za vyombo vya kwenye maji zinaepukika na ndiyo maana anapigana huku na kule katika sakata hilo.
Alisema kuwa lengo lake kubwa ni kuona vyombo vya kuokolea katika kila meli vinapatikana na hasa kwa kutafuta misaada kwa wadau mbali mbali.
“Suala la usalama majini bado haujatiliwa mkazo vya kutosha na jamii pamoja na serikali” alieleza mwanamitindo huyu. “Muda umefika kwa wahusika wote kushirikiana kwa pamoja kuzungumzia na kukabiliana na changamoto hii” alisema Matata.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

MAREHEMU AYOUB MLAY KUAGWA LEO KATIKA KANISA LA KKT MBEZI BEACH.

 Marehemu Ayoub Mlay ataagwa Nyumbani kwake saa 4:30 asubuhi nyumbani kwake TEGETA na baada ya hapo katika kanisa la KKT MBEZI BEACH Kesho Jumanne Saa 6 MCHANA na baada ya kutoa heshima za mwisho, Marehemu atasafirishwa kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa mazishi. Kutakuwa na private cars zitakazo peleka watu moshi kwa aajili ya mazishi mtakao penda kwenda Moshi mnaweza wasiliana na MSEMAJI MKUU WA MAZISHI BWANA SEBASTIAN NDEGE KWA # 0784-888-886.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika nyumba ya marehemu Tegeta, bunde nipatapo picha zaidi nitawawekea kuweza kupata maendeleo ya msiba wa kaka yetu, baba yetu, mjomba yetu marehemu Ayoub Mlay.
Familia ya Marehemu Ayoub enzi za uhai wake na familia yake. Kaacha Mke Jane na watoto watatu Erick, Derick na Michelle.


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

HAPPY BIRTHDAY MR GEORGE KIVARIA KWA KUTIMIZA MIAKA MINGI HAPA DUNIANI.

 Mtoto aliyezaliwa jana George Kivaria Akiwa amepigwa na butwaa baada ya kupewa suprisezzzzz na baadhi ya wafanyakazi wa idara yake wakati alipokumbushwa siku yake ya kuzaliwa hapo jana
 Mh George Kivaria akiwa na furaha wakati wafanyakazi wa idara yake walipomuandalia zawadi ndogo ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake hapo jana japokuwa alikataa kututajia umri wake.
 Suprizeeeeeeee Mtoto aliyezaliwa jana Mh George Kivaria (Wa kwanza Kushoto) akipiga picha keki aliyoletewa na wafanyakazi wa idara yake hapo jana

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

WASANII WAKIKE WAJITOLEA KUTENGENEZA WIMBO UNAOHUSU FISTULA.

wasanii wa kike nchini, wamejitolea kutengeneza wimbo unaowahamasisha wakinamama kujitoa na kuona kama fistula ni ungonjwa ambao upo na una tibika, na kuwahamasisha wakina mama kutokuona aibu na kubaki nao nyumbani. wimbo huo umewashirikisha wasanii kama Mwasiti, Recho, Lina, Vanessa Mdee, Feza Kessy,Keisha, The Trio, Dayna, Maunda Zorro, Pipi, Queen Darlin, Vida, Zuhura, Meninnah, Vumilia,Baby J, Sundy Gaga.usikilize hapa chini.

Via Dj Fetty

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

KINACHOMPONZA PRODYUZA TUDD THOMAS NI UCHAWI AU KUSAHAU?

Prodyuza Tudd Thomas.

MASHABIKI wa mtayarishaji wa muziki (Producer), mwenye uwezo wa kipekee, aliyetayarisha wimbo wa Leka dutigite wa Kigoma All Stars na zingine nyingi, Tudd Thomas, wamekuwa wakiulizana maswali mengi wao kwa wao pasipo kupata majibu.
Safari ya Tudd Thomas katika muziki, ilianzia mkoani Iringa akiwa Iringa Records aliporekodi wimbo wa mwanamuziki Marlaw unaoitwa Bembeleza. Wimbo huo ulipata tuzo ya wimbo bora wa mwaka kutoka Kilimanjaro Tanzania Music Awards mwaka 2008 na pia kumfanya Marlaw apate tuzo ya msanii bora wa kiume kupitia tuzo hizo. Baadae alihamia jijini Dar es Salaam na ndipo alipoonesha uwezo wake zaidi kwa kusuka nyimbo zilizotikisa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Hakuna asiyeufahamu wimbo wa Pii Pii (Missing my baby) wa Marlaw ambao aliutengeneza yeye kupitia Studio ya JML. Wimbo huo ulipata tuzo nyingi ikiwa ni pamoja na tuzo ya Nzumari nchini Kenya mwaka 2009 mbapo uliingia kwenye kipengere cha wimbo bora wa Afrika Mashariki, kumfanya Marlaw aingie kwenye kipengele cha msanii bora wa Afrika Mashariki na kunyakua tuzo hiyo. Baada ya hapo wimbo huo ulipata tuzo ya Kilimanjaro nchini Tanzania kama wimbo bora wa mwaka wa Afro pop mwaka 2010, tuzo ya Chaguo la Teneez Music nchini Kenya kama wimbo ulioongoza kwa kuchukuliwa kwa njia ya mtandao Afrika Mashariki “The most downloaded East African song” mwaka 2010, pamoja na tuzo ya Nigeria Sound City Video Music kama wimbo bora wa Afrika Mashariki mwaka 2010. Aliendelea kutayarisha nyimbo ambazo zilipata umaarufu mkubwa na kuingia kwenye vipengele mbalimbali vya tuzo za muziki za Kilimanjaro. Mwaka 2012, nyimbo tatu zilizotokana na mikono yake zilipata nafasi ya kushiriki tuzo hizo. Nyimbo hizo ni Liz One wa Izzo Business ambao uliingia kwenye vipengele viwili ambavyo ni wimbo bora wa mwaka na wimbo bora wa Hip hop na pia kusababisha msanii huyo aingie kwenye kipengele cha msanii bora wa Hip hop. Milele daima wa Barnaba na Kizunguzungu wa Rachel, ambapo zote ziliingia kipengele cha wimbo bora wa Zouk/Rhumba pia ni nyimbo alizotengeneza mtayarishaji huyo. Nyimbo zingine alizotayarisha ambazo zilifanya vizuri kwenye vituo mbalimbali vya redio na TV ni Kisa pombe na Soldier za Mwasiti, Sorry sana, Mbayuwayu na Mtoto wa Afrika za Marlaw pamoja na Natumaini ya Becka aliyowashirikisha Barnaba na Amin. Pia zipo nyingine kama Unikimbie ya Amin, Tushukuru kwa yote ya Ditto, Lonely ya Linah na Magubegube ya Barnaba. Mtayarishaji huyo ambaye hajawai kuingia kwenye tuzo za Kilimanjaro za muziki wa hapa nchini Tanzania ambazo mwaka huu zimeongezewa kipengele cha Mtayarishaji bora chipukizi ndiye aliyetayarisha wimbo wa Leka dutigite wa Kigoma All Stars kupitia Studio yake ya Ngoma Records. Wimbo huu umeingia kwenye kipengele cha wimbo bora wa mwaka 2013. Pia alishirikiana na mtayarishaji Imma the boy kutengeneza wimbo wa Me ‘n’ U wa Ommy Dimpoz ambao umeingia kwenye kipengele hicho na vipengele vingine ambavyo ni wimbo bora wa Bongo Pop na wimbo bora wa kushirikiana. Alipoulizwa alisema hapendi kuzungumzia juu ya kutotajwa kama miongoni mwa wanaowania tuzo. Aliendelea kusema kwamba, hata kama baadae ikitokea, kwake ni motisha tu, lakini kikubwa zaidi ni kwamba anahisi analo deni kubwa la kutumia uwezo wake ipasavyo kufanya kazi nzuri zaidi ya hapo ili kuutangaza muziki wa Tanzania kimataifa. Pia alisema ana malengo makubwa aliyojiwekea na ndiyo maana kila kukicha anawaza kutayarisha nyimbo zenye tofauti na zenye radha ya kipekee. Tudd Thomas anaendelea kukitumia kipaji chake na ujuzi wake ipasavyo na siku chache zilizopita kuna nyimbo zisizopungua tatu zilizoingia sokoni na zinafanya vizuri, ambazo ni kazi za mikono yake. Nyimbo hizo ni Uswazi take away ya Chegge, Nyumbani ya Kigoma All Stars na pia ameshirikiana kwa kiasi kikubwa na mtayarishaji Fundi Samwel kutengeneza wimbo wa Mahakama ya mapenzi wa Linex.

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

Monday, 20 May 2013

BUNGENI LEO: SUGU ASEMA YEYE SIO MCHOCHEZI.



Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

BREAKING NEWS: JOSE MOURINHO AONDOKA REAL MADRID.

Real Madrid na Jose Mourinho wameingia makubalianao ya kuukatisha mkataba wa kuiongoza timu hiyo ya Spain, Kuna uvumi kuwa Mourinho tayari amekubaliana na Chelsea kuwa kocha wao kwenye msimu ujao wa ligi ya England 


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

MWALIKO WA KUHUDHURIA MDAHALO - READING.

Mustakbal wa Zanzibar (MUWAZA)
UK
 YAH: MKUTANO WA KUZUNGUMZIA MAMBO MUHIMU YA NCHI YETU
Kwa heshima, tafadhali husika na mada ya hapo juu
Nakuletea mwaliko huu kukualika rasmi kwenye mkutano wa kuzungumzia maswala muhimu ya kitaifa yanayotugusa Wa-Tanzania wote.  Mkutano huo utakaofanyika Reading siku ya Jumamosi tarehe 01/06/2013 kuanzia saa 9.00 jioni hadi 12.00 jioni.
Uongozi wa CHADEMA UK, umeonelea kuna umuhimu wa kuwaunganisha Wa-Tanzania kuchambua na kuzungumzia mambo muhimu yanayotuhusu sisi sote. Kwa kufanya hivi tutakuwa tumeruhusu na kuwapa Wa-Tanzania sauti (platform) ya kuyazungumzia maswala mbali mbali kwa uwazi. Hivyo basi tumeandaa mjadala utakaorekodiwa na kurushwa kupitia YouTube channel. Katika mjadala huu, Wa-Tanzania wote wenye mapenzi na nchi yao wanategemewa kuhudhuria bila kujali itikadi, dini, rangi au kabila. Mjadala huu utazungumzia mambo manne ambayo ni UTAIFA; KATIBA; ELIMU; na MUUNGANO. 
Uwakilishi wenu utaongeza chachu na kupeleka ujumbe kwamba waTanzania tulioko UK tuko mstari wa mbele kuyachambua maswala yanayoihusu jamii yetu kwa ueledi mzuri (with maturity) bila kuleta ushabiki wa kidini, kichama, n.k. 
Pamoja na hayo,  kuwepo na jopo (front panel) lenye kazi ya kutoa maoni au majibu yanayotoka kwa Wananchi. Jopo hili litahusisha Wa-Tanzania kutoka Vyama mbali mbali vya kisiasa, Wawakilishi kutoka dini na vikundi mbali mbali hapa UK. Tunategemea kupata Uwakilishi kutoka Serikalini kwa kupitia Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kutokana na hayo, tunachukua fursa hii kukualika wewe na Viongozi wenzio wa Jumuiya yenu  kuhudhuria mjadala huu ambao unatuhusu sisi sote Wa-Tanzania na siyo wa kichama au kidini. Hakutakuwa na nembo au maneno ya kuashiria kwamba hii imeandaliwa na CHADEMA. Hii katika kuonesha nia na madhumuni yaliyopelekea sisi kuandaa mjadala huu kwamba Wa-Tanzania tulioko nje tuna nafasi ya kipekee kuyazungumzia matatizo yetu kwa pamoja bila kujali vikundi ama imani zetu. .
Tunategemea kuwa utashirikiana nasi katika mdahalo huo.
Natanguliza shukurani

Wako mtiifu

Salim SAAD
Mwenyekiti wa Chadema
Tel: +447985290129


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AONGOZA WANANCHI KWENYE MAZISHI YA MZEE SYKES LEO.

Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dk Mohamed Ghalib Bilal, Marais wastaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu Dk Salim Ahmed Salim, Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (aliyesimama kushoto), Mwanasiasa mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru (aliyeketi kulia)  wakiungana na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya Mzee Ally Kleist Sykes, mmoja wa waasisi wa chama cha TANU, leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo Mei 20, 2013
Rais Jakaya Kikwete akiongoza akiweka udongo kaburini wakati wa mazishi hayo.  
Rais Jakaya Kikwete akiongoza mamia ya waombolezaji katika kuomba dua wakati wa mazishi ya mwasis huyo gwiji.


Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Mixed Posts