Friday, 6 July 2012

KASEBA VS CHEKA NANI ZAIDI UWANJA WA TAIFA KESHO...!!!


Bondia Japhet Kaseba kushoto na Francis Cheka wakionyeshana umwamba wa kila mmoja kutaka kumchakaza mwezake wakati walipopima uzito leo kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika katika uwanja wa taifa siku ya jumamosi katikati ni mratibu wa mpambano huo Kaike Siraju.

Baadhi ya Mabondia na Makocha wakisubiri kupima uzito kwa mabondia kwa ajili ya Mpambano wa siku ya sabasaba katika tamasha la matumaini.
Bondia Francis Cheka akipima uzito kwa ajili ya kumkabili mpizani wake Japhet Kaseba kesho katika uwanja wa Taifa wakati wa Tamasha la matumaini ambapo kutakuwa na burudani mbalimbali mbali 
Mratibu wa mpambano wa ngumi Kaike Siraju katikati akiwainua mikono juu mabondia Japhet Kaseba kushoto na Francis Cheka baada ya kumaliza kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika siku ya sabasaba katika uwanja wa taifa wakati wa Tamasha la Matumaini kwa watanzania litakalokusanya burudani mbali mbali.
Bondia kutoka Kambi ya Ilala Ibrahimu Class akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Sadiki Momba utakaofanyika Kesho katika uwanja wa Taifa
 Bondia toka kambi ya Ilala Ibrahimu Class akipima Afya kwa ajili ya mpambano wake na Sadiki Momba utakaofanyika kesho katika uwanja wa taifa
 
Bondia Francis Cheka akipima Afya kwa ajili ya mpambano wake na Japhert Kaseba utakaofanyika kjesho katika uwanja wa Taifa. 

Stay connected with Jestina-George.com, follow us on Twitter and Facebook for all the latest fashion trends, latest celebrity news, gossip, showbiz & current affairs

0 comments/maoni:

Post a Comment

Toa maoni yako kwa uhuru na tafadhali naomba usichafue hali ya hewa humu ndani wala kujeruhi hisia za mtu au watu. (Let's please maintain a high level of discipline! Zero tolerance policy on abussive language!) Asante na karibu sana.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Mixed Posts